Mabingwa wa sasa wa soka barani Afrika TP Mazembe, wamesema watakata rufaa kutokana na uamuzi wa Shirikisho la Kandanda Afrika- Caf, kuiondoa katika Ligi ya Ubingwa wa Vilabu kutokana na kumchezesha mchezaji asiyestahiki.
Katika taarifa iliyotolewa muda mfupi baada ya uamuzi wa Kamati ya Maandalizi ya Caf kwa mashindano ya vilabu, klabu hiyo ya Congo imesisitiza haijavunja sheria kwa kumchezesha Janvier Besala Bokungu, ambaye klabu ya soka ya Simba ya Tanzania imemshutumu alivunja mkataba wake na klabu ya Esperance na kujiunga na Mazembe, hali iliyomfanya asistahili kucheza katika michuano ya Caf.
“Uongozi wa Mazembe unauona uamuzi wa Caf haukubaliki ndio maana haraka tutakata rufaa kutokana na uamuzi huo. Meneja wetu Mkuu Frederick Kitenge kwa sasa yupo Cairo akiangalia vipengele vyote vya kupata haki kwa klabu yetu,” Taarifa hiyo ya Caf imesomeka katika mtandao rasmi wa Corbeaux.
Iwapo rufaa ya Mazembe itagonga mwamba, watakosa nafasi ya kutetea ubingwa wao na pengine kuweka rekodi ya kuwa mabingwa wa vilabu barani Afrika kwa mwaka wa tatu mfululizo, ambapo klabu hiyo imesema ndio lengo lao kuu msimu huu.
Katika hali nyingine, Chama cha taifa cha kandanda cha Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, kimetupilia mbali maombi ya Mazembe ya kutaka kuahirishwa mechi yake ya mwishoni mwa wiki dhidi ya DCMP, kwa sababu mabingwa hao wana ziara ya mazoezi nchini Brazil.
DCMP itadai pointi zote tatu iwapo Mazembe haitatokea uwanjani siku ya Jumapili. Kuna mashaka kama timu hiyo itasafiri kuelekea Marekani Kusini ili ikabiliane na DCMP.
Who doesn't remember a song Vijimambo? I bet even 10 year olds back then leave alone 50 year olds were chanting with Noorah on this. Well he is doing it again...Lugha Gongana is track that shows a funny side of life of a girl who has fallen deeply in love with a guy who doesn't have a first clue of English language and may be even romance as well...it's even sad sometimes how this guy is missing out a chance to be intimate with this girl and the girl with the guy because of small but important difference...the language
Hermy B produced the track, it is the first Noorah - Hermy B collaboration but the creative writing was done entirely by Noorah himself. Don’t get it twisted and ask why have we not spoken of the girl’s voice in this song, all vocals were laid down by Noorah himself with help of state of the art technology that can only be found at B’Hits studios. It is definitely going to be a good year for Noorah as he is going back to the Roots, and a Blessed year for B’Hits as well just because it’s B'HITS.